UTUNZAJI WA SHAMBA NA MIMEA.
(a) Uwekaji wa matandazwa
Kazi hii ni vyema ikafanywa mara baada ya kupanda kama inawezekana.
Matandazo yawe ni makavu na unene wa sentimeta 15 ili kuhifadhi
unyevu, kuzuia magugu na yakioza yataongeza mbolea.
(b) Uongezaji wa mbolea
Baada kupanda ni vyema kuongeza mbolea madebe 2 kuzunguuka shina
la migomba kila baada ya miaka miwili au mitatu. Mbolea hii inatakiwa
kuchanganywa na udongo na kufunikwa kwa matandazwa.
(c) Umwagiliaji maji shambani
Migomba huhitaji maji mengi. Wakati wa kiangazi. Inafaa kumwagilia ili
kuto kupunguza sana ukubwa na wingi wa ndizi zinazotarajiwa kuvunwa
kwa mwaka. Kiasi cha maji kinachotakiwa kwa wiki ni milimita 25,
yaani eneo linalo zunguka shina la migomba lilowe kabisa.
(d) Kupunguzia machipukizi
Inatakiwa kupunguza mimea ya migomba kwa kila shina na kubaki
mimea mitatu tu, yaani Mgomba wenye ndizi (Mama), Mgomba
mkubwa ambao bado haujazaa lakini unakaribia kuchanua (Mtoto),
Mgomba mchanga uliochipua hivi karibuni ( Mjukuu)
(e) Uondoaji wa Majani Makavu
Mimea ya migomba inafaa iondolewe majani yote makavu ili kuondoa
uwezekano wa kuwepo mazalia ya wadudu na magonjwa, kuruhusu
mionzi ya jua na kufanya urahisi wa kuhudumia shamba .Pia hufanya
shamba kuonekana safi.
(f) Uondoaji wa ncha mwishoni mwa matunda
Baada ya mkungu kutoa ndizi, ua hunyauka na kubakiza ncha mwishoni
mwa matunda. Ncha hizo hupaswa kuondolewa .Huduma hii husaidia
kupunguza uwezekano wa kujeruhi matunda wakati wa kusafirisha
jambo ambalo kupunguza ubora wa tunda.
(g) Kuweka Miega
Miega ni nguzo au kamba ambazo hutumika kuzuia migomba iliyobeba
mikungu mikubwa isianguke kutokana na uzito mkubwa. Miega ni ya
lazima katika sehemu zenye upepo mkali. Kazi hii inatakiwa kufanywa
kwa uangalifu ili isijeruhi ndizi na mgomba wenyewe.
(h) Uondoaji wa kichombezo cha ua la kiume (Shumba)
Uondoaji wa shumba huwezesha matunda kukua vizuri, kuongezeka
uzito wa mkungu pia huzuia magonjwa kama vile ugonjwa wa mnyauko
wa migomba (Banana Baterial Wilt), ugonjwa wa Majivu nchani mwa
matunda (Cigar end rot). Ukataji hufanyika juu ya kovu la pili baada ya
kichana cha mwisho, kwa kutumia kisu kikali.
UVUNAJI
Zao la ndizi huweza kuanza kuvunwa katika kipindi cha miezi 9 hadi
miezi 15 tangu kupandwa kwa chipukizi. Muda wa kuvunwa hutegemea
hali ya hewa. Katika sehemu za joto ndizi huvunwa mapema zaidi kuliko
sehemu za baridi. Pia migomba iliyopandwa kwa kutumia machipukizi
huzaa mapema kuliko iliyopandwa miche iliyozalishwa kwa chupa
(tissue culture)
MATUMIZI YA RIBONI
Riboni za rangi moja (au alama ya kamba) hufungwa kwenye migomba
ya umri mmoja mara tu inapoanza kuchanua, na riboni ya rangi nyingine
hufungwa kwenye migomba itakayoanza kuchanua wiki mbili hivi
zinazofuata na kuendelea hivyo ili kurahisisha kuitambulisha mikungu
ambayo itavunwa kwa wakati mmoja. Pia matumizi ya riboni hurahisiha utunzaji wa kumbukumbu ili kujua ni lini na ni mikungu mingapi itavunwa.
WAKATI UNAOFAA KUVUNA
Mkungu wa ndizi huweza kuvunwa katika hatua tofauti kulingana na matumizi, aina na mahitaji ya soko. Mkungu huachwa kwenye mgomba mpaka vidole (matunda ) vimejaa. Uzito wa mkungu hongezeka haraka
katika wiki mbili za mwisho, ambapo migongo ya ndizi hutoweka.
Ndizi zinaweza kuvunwa zikiwa zimekomaa na zimeiva kwa kiasi cha asilimia 75 kwa ajili ya kusafirishwa mbali, pia zinaweza kuvunwa zikiwa kukomaa na zimeanza kuiva kwa ajili ya soko la karibu, au zikiwa
zimekomaa na kuiva kabisa kwa ajili ya soko na matumizi ya nyumbani
Njia bora ya kukata mkungu, ni ile inayohakikisha kuwa mkungu wa ndizi hauanguki chini na kuvunja, kuchubuan au kuharibu ndizi, jambo ambalo litapunguza ubora. Ukichelewa kuvuna ndizi zinaweza kuharibiwa na ndege, wanyama, wadudu au kuibiwa.
UBORA WA NDIZI
Ndizi zenye sifa nzuri sokoni ni zile ambazo zimekomaa kwa kiasi
kinachotakiwa na zenye vidole vyenye urefu mzuri na visivyo na
michubuko. Pia ziwe hazijashambuliwa na magonjwa wala wadudu
waharibifu.
KIASI CHA MAVUNO
Mavuno ya ndizi hutegemea zaidi aina ya migomba, hali ya hewa, utunzaji wa mimea shambani. Mavuno huweza kufikia hadi tani 60 au zaidi kwa hekta kwa mwaka. Hata hivyo mavuno mazuri kwa mkulima
wa kawaida yasipungue kati ya tani 20 hadi 30 kwa hekta kwa mwaka.
MAGONJWA
Ugonjwa wa hatari sana ulioingia hivi karibuni katika wilaya ya Muleba
na maeneo mengine mkoani Kagera kutoka nchi jirani ya Uganda ni wa
Mnyauko wa migomba unaosababishwa na bakteria (Banana Bacterial
Wilt). Magonjwa mengine yanayosumbua zao hili ni Kuoza tunguu,
Ugonjwa wa panama, Ugonjwa wa majivu nchani mwa tunda, Sigatoka,
na Moko.
WADUDU WAHARIBIFU
Wadudu wanaosumbua zaidi hili ni Minyoo fundo (Banana nematodes),
na Vifukuzi (Banana weevils).
UDHIBITI WA MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU
Magonjwa na wadudu hawa huweza kuepukwa kwa kufuata kanuni bora
za uzalishaji wa zao hili. kama usafi wa shamba na kuchagua chipukizi
bora. Au kupanda miche iliyozalishwa kwa chupa (Tissue culture banana
seedlings) Hata hivyo mara mataizo haya yakitokea muone mtaalam wa
kilimo aliye karibu ili aweze kukupa ushauri.
(a) Uwekaji wa matandazwa
Kazi hii ni vyema ikafanywa mara baada ya kupanda kama inawezekana.
Matandazo yawe ni makavu na unene wa sentimeta 15 ili kuhifadhi
unyevu, kuzuia magugu na yakioza yataongeza mbolea.
(b) Uongezaji wa mbolea
Baada kupanda ni vyema kuongeza mbolea madebe 2 kuzunguuka shina
la migomba kila baada ya miaka miwili au mitatu. Mbolea hii inatakiwa
kuchanganywa na udongo na kufunikwa kwa matandazwa.
(c) Umwagiliaji maji shambani
Migomba huhitaji maji mengi. Wakati wa kiangazi. Inafaa kumwagilia ili
kuto kupunguza sana ukubwa na wingi wa ndizi zinazotarajiwa kuvunwa
kwa mwaka. Kiasi cha maji kinachotakiwa kwa wiki ni milimita 25,
yaani eneo linalo zunguka shina la migomba lilowe kabisa.
(d) Kupunguzia machipukizi
Inatakiwa kupunguza mimea ya migomba kwa kila shina na kubaki
mimea mitatu tu, yaani Mgomba wenye ndizi (Mama), Mgomba
mkubwa ambao bado haujazaa lakini unakaribia kuchanua (Mtoto),
Mgomba mchanga uliochipua hivi karibuni ( Mjukuu)
(e) Uondoaji wa Majani Makavu
Mimea ya migomba inafaa iondolewe majani yote makavu ili kuondoa
uwezekano wa kuwepo mazalia ya wadudu na magonjwa, kuruhusu
mionzi ya jua na kufanya urahisi wa kuhudumia shamba .Pia hufanya
shamba kuonekana safi.
(f) Uondoaji wa ncha mwishoni mwa matunda
Baada ya mkungu kutoa ndizi, ua hunyauka na kubakiza ncha mwishoni
mwa matunda. Ncha hizo hupaswa kuondolewa .Huduma hii husaidia
kupunguza uwezekano wa kujeruhi matunda wakati wa kusafirisha
jambo ambalo kupunguza ubora wa tunda.
(g) Kuweka Miega
Miega ni nguzo au kamba ambazo hutumika kuzuia migomba iliyobeba
mikungu mikubwa isianguke kutokana na uzito mkubwa. Miega ni ya
lazima katika sehemu zenye upepo mkali. Kazi hii inatakiwa kufanywa
kwa uangalifu ili isijeruhi ndizi na mgomba wenyewe.
(h) Uondoaji wa kichombezo cha ua la kiume (Shumba)
Uondoaji wa shumba huwezesha matunda kukua vizuri, kuongezeka
uzito wa mkungu pia huzuia magonjwa kama vile ugonjwa wa mnyauko
wa migomba (Banana Baterial Wilt), ugonjwa wa Majivu nchani mwa
matunda (Cigar end rot). Ukataji hufanyika juu ya kovu la pili baada ya
kichana cha mwisho, kwa kutumia kisu kikali.
UVUNAJI
Zao la ndizi huweza kuanza kuvunwa katika kipindi cha miezi 9 hadi
miezi 15 tangu kupandwa kwa chipukizi. Muda wa kuvunwa hutegemea
hali ya hewa. Katika sehemu za joto ndizi huvunwa mapema zaidi kuliko
sehemu za baridi. Pia migomba iliyopandwa kwa kutumia machipukizi
huzaa mapema kuliko iliyopandwa miche iliyozalishwa kwa chupa
(tissue culture)
MATUMIZI YA RIBONI
Riboni za rangi moja (au alama ya kamba) hufungwa kwenye migomba
ya umri mmoja mara tu inapoanza kuchanua, na riboni ya rangi nyingine
hufungwa kwenye migomba itakayoanza kuchanua wiki mbili hivi
zinazofuata na kuendelea hivyo ili kurahisisha kuitambulisha mikungu
ambayo itavunwa kwa wakati mmoja. Pia matumizi ya riboni hurahisiha utunzaji wa kumbukumbu ili kujua ni lini na ni mikungu mingapi itavunwa.
WAKATI UNAOFAA KUVUNA
Mkungu wa ndizi huweza kuvunwa katika hatua tofauti kulingana na matumizi, aina na mahitaji ya soko. Mkungu huachwa kwenye mgomba mpaka vidole (matunda ) vimejaa. Uzito wa mkungu hongezeka haraka
katika wiki mbili za mwisho, ambapo migongo ya ndizi hutoweka.
Ndizi zinaweza kuvunwa zikiwa zimekomaa na zimeiva kwa kiasi cha asilimia 75 kwa ajili ya kusafirishwa mbali, pia zinaweza kuvunwa zikiwa kukomaa na zimeanza kuiva kwa ajili ya soko la karibu, au zikiwa
zimekomaa na kuiva kabisa kwa ajili ya soko na matumizi ya nyumbani
Njia bora ya kukata mkungu, ni ile inayohakikisha kuwa mkungu wa ndizi hauanguki chini na kuvunja, kuchubuan au kuharibu ndizi, jambo ambalo litapunguza ubora. Ukichelewa kuvuna ndizi zinaweza kuharibiwa na ndege, wanyama, wadudu au kuibiwa.
UBORA WA NDIZI
Ndizi zenye sifa nzuri sokoni ni zile ambazo zimekomaa kwa kiasi
kinachotakiwa na zenye vidole vyenye urefu mzuri na visivyo na
michubuko. Pia ziwe hazijashambuliwa na magonjwa wala wadudu
waharibifu.
KIASI CHA MAVUNO
Mavuno ya ndizi hutegemea zaidi aina ya migomba, hali ya hewa, utunzaji wa mimea shambani. Mavuno huweza kufikia hadi tani 60 au zaidi kwa hekta kwa mwaka. Hata hivyo mavuno mazuri kwa mkulima
wa kawaida yasipungue kati ya tani 20 hadi 30 kwa hekta kwa mwaka.
MAGONJWA
Ugonjwa wa hatari sana ulioingia hivi karibuni katika wilaya ya Muleba
na maeneo mengine mkoani Kagera kutoka nchi jirani ya Uganda ni wa
Mnyauko wa migomba unaosababishwa na bakteria (Banana Bacterial
Wilt). Magonjwa mengine yanayosumbua zao hili ni Kuoza tunguu,
Ugonjwa wa panama, Ugonjwa wa majivu nchani mwa tunda, Sigatoka,
na Moko.
WADUDU WAHARIBIFU
Wadudu wanaosumbua zaidi hili ni Minyoo fundo (Banana nematodes),
na Vifukuzi (Banana weevils).
UDHIBITI WA MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU
Magonjwa na wadudu hawa huweza kuepukwa kwa kufuata kanuni bora
za uzalishaji wa zao hili. kama usafi wa shamba na kuchagua chipukizi
bora. Au kupanda miche iliyozalishwa kwa chupa (Tissue culture banana
seedlings) Hata hivyo mara mataizo haya yakitokea muone mtaalam wa
kilimo aliye karibu ili aweze kukupa ushauri.
- Dalili za ugonjwa wa mnyauko wa migomba unaosababishwa na bakteria